Bismillahi Rahmani Rahiim
Ifuatayo ni baadhi ya misikiti iliyovunjwa na Mawahabi katika mji wa Madina.
Masjid Bany Quraydhwa:
Katika mji wa Madina kulikua na msikiti unaojulikana kwa jina ( Masjib bany quraydhwa ), umepewa jina hilo kwasababu Mtume (s.a.w) aliswali sehemu hiyo alipokua amewazunguka Banuu Quraydhwa.
Na ametaja Ibnu Shabah na Ibnu Najjaar na Alhaythamy na wengineo sehemu ya huo msikiti, na kisa cha Mtume (s.a.w) kuswali katika hio sehemu ni mashuhuri kama ilivyo kuja katika hadithi ya Abu Said Alkhudury (r.a.3), kimepokewa na Imam Bukhary na Imam Muslim.