Saturday, January 19, 2013

MISIKITI YA MADINA WALIYOVUNJA MAWAHABI


Bismillahi Rahmani Rahiim

Ifuatayo ni baadhi ya misikiti iliyovunjwa na Mawahabi katika mji wa Madina.

Masjid Bany Quraydhwa:
Katika mji wa Madina kulikua na msikiti unaojulikana kwa jina ( Masjib bany quraydhwa ), umepewa jina hilo kwasababu Mtume (s.a.w) aliswali sehemu hiyo alipokua amewazunguka Banuu Quraydhwa.

Na ametaja Ibnu Shabah na Ibnu Najjaar na Alhaythamy na wengineo sehemu ya huo msikiti, na kisa cha Mtume (s.a.w) kuswali katika hio sehemu ni mashuhuri kama ilivyo kuja katika hadithi ya Abu Said Alkhudury (r.a.3), kimepokewa na Imam Bukhary na Imam Muslim.

Sunday, January 6, 2013

Kwanini Tunasherehekea Mawlid?




SABABU ISHIRINI NA TANO ZINAZOMFANYA MUISLAMU ASHEREHEKEE MAZAZI YA MTUME (Swalallahu aleihi wa Salaam)

1: Mawlid ni kuonesha kumfurahikia Mtume (Swalallahu aleihi wa salaam), na kufurahikia mazazi ya Mtume swalallahu aleihi wa salaam kulimnufaisha kafiri, jee sisi waislamu?! na hio ni dalili aloitumia Ibnu hajar katika fathul bary v9 p145 aliposema:
وذكر السهيلي أن العباس بن عبد المطلب رضي الله عنه قال : لما مات أبو لهب رأيته في منامي بعد حول في شر حال فقال ما لقيت بعدكم راحة الا أن العذاب يخفف عني كل يوم اثنين قال وذلك أن النبي صلى الله عليه وسلم ولد يوم الإثنين وكانت ثويبة بشرت أبا لهب بمولده فاعتقها .