Monday, January 30, 2012

Al-Qaswidatu Mudhwariyah Fiy Swalat 3ala Khairul Bariyah



Mawlāya šalli wa sallim dāiman abadan
 'Alā Ĥabībika Khayril khalqi kullihim

Yā Rabbi šalli ‘alāl Mukhtāri min Muđarin
wal Anbiyā wa jamī’ir Rusli mā dhukirū


Wa šalli Rabbi ‘alāl Hādī wa Shī’atihi
wa Šaĥbihi man li ťayyid Dīni qad nasharū

Sunday, January 29, 2012

Sherehe za uhuru Zanzibar, 1963

December 1963, siku ya sherehe za uhuru wa Zanzibar. 

Habib Umar bin Sumayt
  akiwa mstari wa mbele kwa heshima, nyuma (kwenye kiti) ni Qadhi mkuu, Shaykh Abdallah Saleh al-Farsi, ambaye alikuwa  mwanafunzi mkuu wa Habib Umar bin Sumayt.

1962: Jumuiya ya Waislamu Mnazi Mmoja

Picha ya Ukumbusho, iliyopigwa Dar-es-Salaam 1962, mbele ya Jumuiya ya Waislamu Mnazi Moja DSM, kwa ajili ya kuweka jiwe la Msingi la Masjid Kitumbini (Msikiti Mkuu wa Ijumaa DSM), ambapo Habib Umar na ujumbe wake kutoka Zanzibar na Mombasa walkwenda kufanya shguhuli hiyo.

Picha ya pamoja ya mashaykh (1962)

Habib Umar bin Sumayt na Habib Ahmad bin Hussayn Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim walipomtembelea Balozi Abbas Syks, nyumbani kwake 1962, baada ya kuweka jiwe la msingi la Masjid Kitumbini, DSM. 

Baadhi ya majina ya waliomo katika picha hii ni kama ifuatavyo: 1. Shareef Abdulkader al-Juinaydi (DSM), 2.al-'Allamah al-'Arif Billah Habib Ahmad bin Husayn Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim (znz); 3. Balozi Abbas Syks (DSM); 4. al-Allamah al-'Arif Billah Habib Umar bin Ahmad bin Sumayt (znz);5. al-'Allamah al-Fadhil Shaykh Hassan bi 'Amier (znz) Mufti wa Tanganyika; 6. al-'Allamah Habib Hamid Mansab Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim (znz); 7; al-'Allamah Sayyid Ali Badawi (Lamu-znz); 8. al-'Allamah Maallim Sa'id bin Ahmad (Mombasa); 9. al-Akh Muhammad 'Alwi Bu Numay (znz); 10. al-Akh Abdulwahhab (DSM) presidant of Arab Association Tanganyika; 11. Shaykh al-Fadhil Abdulkader Ba'Abbad (DSM). 12. Shaykh Qasim bin Jum'a Darwesh (DSM).

Ma Habaib wakiwa kwa Balozi Abbas Sykes (1962)

Nyota mbili kubwa za ZNZ, al-Habib al-'Allamah al-'Arif billah Sayyyid Ahmad bin Husayn Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim na al-Habib al-'Allama al-'Arif Billah Sayyid Umar bin Abi Bakr bin Sumyat wakiwa nje ya nyumba ya Balozi Abbas Syks (Mkuu wa Mkoa wa DSM, wakati huo-amesimama nyuma yao) walipokwenda kumtembelea nyumbani kwake DSM, baada ya kuweka jiwe la msingi la Msikitu Mkuu wa Ujumaa DSM, 1962.

Habib Umar na Habib Ahmad bin Hussayn walialikwa rasmi na Jumuiya ya Msikiti wa Ijumaa kwendakuwekajiwe la msingi la kuupanua msikiti huo na kuwa Msikiti Mkuu wa Ijumaa.

1965: Mashaykh wakiwa Sharif-Msa, Zanzibar

Mrithi wa Habib Umar bin Sumayt: al-Habib al-‘Allama Hamid Mansab alliyevaa bushti, akiwa katika picha ya pamoja kwenye shamba la Habib Umar bin Sumayt lijulikanalo kwa jina la Sharif-Msa ZNZ 1965. Baadhi ya waliyomo na majina yao, kama ifuatavyo:

1. Maallim Saleh; 2. Habib Umar bin Abdallah Mwinyi Baraka; 3. Habib Ali Badawi; 4. Habib Hamid Mansab Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim; 5.Haabib Abdulwahid bin Muhammad Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim; 6. Habib Ahmad bin Hamid Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim; 7. Habib Ahmad Yaasin Jamalullayl; 8. Sayyid Johari Jamallulayl; 9. Shaykh Ilyas; 10. Habib Muhammad Alwi Bunumayy; 11. Habib Umar bin Alwi Bunumayy.


Saturday, January 28, 2012

Kwanini msikiti wa Makka ukaitwa Masjid Al Haram?


SWALI:


Neno HARAM na HARAAM yana maana tofauti au ni maana moja tu (kinyume cha halali)? Does it mean "Holy/Sacred" also? Na kwanini msikiti wa Makka ukaitwa Masjid Al Haram?
----------------------------------------------------------------------------------------------

JIBU:

Bismillah, wa Sallah Allah ala Rasul Allah!

Zanzibar Muslim Academy --1960's




Kutoka kulia kwenda kushoto: Waliokaa: wa kwanza ni Sayyid Ahmad Hamid Mansab Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim (alikuwa akisomesha Nahw, na Sarf); wa pili kutoka kulia ni Al-ällama alkabir Sheikh Sulaiman bin Muahammad Al-Alawi - huyu bwana ni mwalimu wa karibu maulamaa wote wa Zanzibar na nchi jirani za Afrika ya Mashariki- alilkuwa bahari isiyo na fukwe kwenye elimu mbali mbali. Yeye alisomesha Fiqh; Arudhi (elimu ya fani ya kutunga mashairi ya Kiarabu); Balagha na kadhalika. Ni shida, kama si muhali, kumpata mwana chuoni ye yote katika Afrika ya Mashariki, Kati na Kusini, asiwe mwanafunzi wa Maulana huyu: Allah yarhamhu. Maisha yake yote yalikuwa katika kusomesha dini tu, tokea anaamka hadi anakwenda kulala. Msikiti Gofu ulikuwa ndio mahali anaposomesha kuanzia baada ya sala ya Alfajiri, hadi baadaye kwenda Muslim Academy, na akirudi baada ya sala ya Adhuhuri hadi baada ya sala ya Isha. Allah yarhamhu wa yuskinuhu al-Janna.

Wa tatu kutoka kulia na Sayyid Umar bin Abdallah Ibn Shaykh Abi Bakr bin Salim (Mwinyi Baraka). Yeye alikuwa Mwalimu Mkuu wa Muslim Academy. Wa nne kutoka kulia ni Sayyid Abdurrahman bin Hamid Al-Sirry - Huyu Bwana alikuwa bahari katika elimu za Lugha, Mashairi na fani nyengine. Yeye alisomesha Arabic Literature (al-Adab al-Arabiyy).

Wa tano kutoka kulia ni Sayyid Ali Badawi Jamalullayl- huyu Bwana alikuwa alim mkubwa sana. Alisomesha Jiographia ya Nyota, Sayari na Ardhi. Vile vile alisomesha Elimu ya Maani na Balagha.

Tawassul Katika Sunnah....



Tawassul katika Sunnah Pt.1



Tawassul katika sunnah Pt. 2

By: Ustadh Mbarak Ahmed.


Thursday, January 26, 2012

Ratib Al Haddad

Ratib Al Haddad

Ya

SAYYIDUNĀ AL-IMĀM QUTB U’L IRSHĀD
AL-HABĪB ‘ABDALLĀH BIN ‘ALAWĪ AL-HADDĀD
Rady Allāhu ‘Anhu (1044-1132 H)

.

Johari za wanazuoni


"Tukana upendavyo ewe dhalili kumyamazia mjinga, ndiyo jawabu!

Sikuishiwa maneno hata qalili! . ila tokeani simba, mbwa kumjibu?!"


~  
Imam Shafi'i--Rahimahullah

Misingi ya madhehebu ya sunni

Swali:
Nini tofauti kuu za kimsingi katika fiqh ya madhhab ya Hanafi, Maliki, Shafi, na Hanbali?

Jibu:   Misingi ya madhehebu ya imam Abu hanifa:

1: Qur'an.

2: sunnah.

3: Aqwaal za maswahaba.

4: Ijmaa3.

Swali kuhusu Eda...

SWALI:

Hivi kila mara tunazungumzia kukaa eda!
Je hiyo Edda inakaliwa vipi?
Nini masharti ya Edda au kuna mavazi maalum ambayo yanatakiwa kuvaliwa??
Je kunatofauti ya hizi edda mbili ( ya kufiwa na kuachwa) zaidi ya kupishana siku kama mwanamke si mjamzito??
Naombeni kufahamishwa kiundani juu ya hili tafadhali! : 

-----------------------------------------------------------------------------------------------

MAJIBU, kwa muhtasari:

Eda ni muhula maalum aliouweka Mwenyezi Mungu, kwa mwanamke aliyefiwa na mumewe, katika ndoa halali, au aliyetalikiwa ndani ya ndoa halali. Muhula huo ama ni wa uja uzito, au Tohara za hedhi, au miezi. 

Hivyo, sababu ya Eda ni mbili; 1. Kufiwa na mume au 2. Kuachwa kwa talaka.

Tawassul


Video: Tawassul katika Qur'an...
By: Sidi Mbarak Ahmed

Tizama sehemu zinazofuatia kwenye link zifuatazo
http://www.youtube.com/watch?v=N3OPf5NkfzQ&feature=related (pt 2)

http://www.youtube.com/watch?v=NFwRMSG6SKI&feature=related (pt 3)

ALLAH is NOT an object...


ALLAH (s.w.t) is Unlike ANYTHING
ALLAH IS NOT AN OBJECT 

The Qur’an informs us in Suratush-Shura, 11:

“There is absolutely nothing like Allah whatsoever.”

This Verse contains the meaning that Allah absolutely and categorically does not resemble any of the creations.  This means that Allah is not similar to the humans, the jinn, the Angels.  Allah is not similar to the heavens, the celestial bodies, the earth, Paradise, or anything that exists therein. 

Wednesday, January 25, 2012



Sayyid Al Habib Umar bin Hafiz (Allah amhifadhi) aliulizwa:

"Tufanyeje tukiona uvivu na ukosefu moyo wa kufanya baadhi ya sunnah na nyiradi?"


Akajibu: "Mjisukume mbele kwa kujitia moyo (matumaini): mjikumbushe malipo ya amali hizo na matokeo yake (faida) katika maisha yajayo.

Ukijiona mvivu wakati mwingine usikate tamaa. Usiwache kufanya (hilo jambo) na usilicheleweshe - jirudi ufanye ulivyokuwa ukifanya, kwa kuwa ki asili, haujakamilika.

Huenda uvivu wako unakufundisha somo kubwa na muhimu. Unaweza ukakuletea/jengea udhoofu na unyenyekevu mbele ya Allah, na unaweza kukuondolea 'ujub rohoni mwako. Hii yaweza kuwa na faida zaidi kwako kuliko kufanya kitendo chenyewe"

Tuesday, January 24, 2012




Video: Umuhimu wa kunufaisha wenzako

By: Mbarak Ahmed.

Monday, January 23, 2012

Qur'an [91:7 - 10] Surat Ash-Shams (Jua) - سورة الشمس


91:8


91:9


91:7


91:10


 

"Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza! 
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake, Hakika amefanikiwa aliye itakasa, Na hakika amekhasiri aliye iviza."