Friday, March 23, 2012

Bukhari, 1:2


Sahih Al-Bukhari: Kitabu #1, Hadith #2

Narrated 'Aisha:
(the mother of the faithful believers) Al-Harith bin Hisham asked Allah's Apostle "O Allah's Apostle! How is the Divine Inspiration revealed to you?" Allah's Apostle replied, "Sometimes it is (revealed) like the ringing of a bell, this form of Inspiration is the hardest of all and then this state passes off after I have grasped what is inspired. Sometimes the Angel comes in the form of a man and talks to me and I grasp whatever he says." 'Aisha added: Verily I saw the Prophet being inspired divinely on a very cold day and noticed the sweat dropping from his forehead (as the Inspiration was over).


حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، قَالَ أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها ـ أَنَّ الْحَارِثَ بْنَ هِشَامٍ ـ رضى الله عنه ـ سَأَلَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ كَيْفَ يَأْتِيكَ الْوَحْىُ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " أَحْيَانًا يَأْتِينِي مِثْلَ صَلْصَلَةِ الْجَرَسِ ـ وَهُوَ أَشَدُّهُ عَلَىَّ ـ فَيُفْصَمُ عَنِّي وَقَدْ وَعَيْتُ عَنْهُ مَا قَالَ، وَأَحْيَانًا يَتَمَثَّلُ لِيَ الْمَلَكُ رَجُلاً فَيُكَلِّمُنِي فَأَعِي مَا يَقُولُ ". قَالَتْ عَائِشَةُ رضى الله عنها وَلَقَدْ رَأَيْتُهُ يَنْزِلُ عَلَيْهِ الْوَحْىُ فِي الْيَوْمِ الشَّدِيدِ الْبَرْدِ، فَيَفْصِمُ عَنْهُ وَإِنَّ جَبِينَهُ لَيَتَفَصَّدُ عَرَقًا.


Amesimulia 'Aisha (Mama wa waumini) (r.a):
Al Harith bin Hisham alimuuliza Mjumbe wa Allah (s.w.t) "Ewe Mjumbe wa Allah! Ni vipi unafunuliwa (unaletewa) wahyi?" Mjumbe wa Allah (s.a.w) akamjibu, "Wakati mwingine huja kama mlio wa kengele, aina hii ya wahyi ni ngumu (nzito) zaidi ya yote halafu hali hiyo hupita baada ya kuelewa nilicholetewa. Wakati mwingine yeye Malaika huja katika umbile la mwanadamu na kuzungumza nami na mimi huelewa chochote anachosema" Aisha (r.a) akaongezea: Kwa hakika nilimuona Nabii akipokea wahyi siku ya baridi kali na halafu nikaona jasho likimtoka kwenye paji la uso wake"

3 comments:

  1. Hadithi hii inazungumzia njia alizokua akiletewa wahyi bwana Mtume s.a.w. nazo ni njia mbili, yakwanza: humjia kama sauti za kengele. yapili: akimjia jibriil kwa sura ya mtu kisha akimpa wahyi. na kwa njia zote hizi mbili alikua akiletewa na jibriil a.s.

    Njia yakwanza ilikua nzito kushinda yapili, shekhe letu alkittaany asema ndio ilikusudiwa katika aya inayosema: كِتَابٌ أُنْزِلَ إِلَيْكَ فَلَا يَكُنْ فِي صَدْرِكَ حَرَجٌ مِنْهُ , kitabu ulichoteremshiwa basi kusiwe katika kifua chako uzito. baadhi wamefasiri kua 7araj hapa maana yake ni shaka, na hasha kifua cha Mtume s.a.w kiwe na shaka na Qur'an. shekhe asema minhu hapa imekusudiwa hii sampuli yakwanza ya wahyi ambao unakuja kwa sura ya sauti za kengele, ulikua ni mzito kwake, na ndio mwisho wa hadithi nana aisha r.a.3 akasema mpaka anatokwa na jasho katika masiku ya baridi kali! Na sampuli hii ya wahyi ndio ikamfaya Allaah s.w amfungulie kifua chake kiweze kuhimili uzito wa Qur'an aliposema: ألم نشرح لك صدرك , hatukukikunjua kifua chako! aya hii imekuja baada ya kuzungumziwa wahyi katika sura iloitangulia ambayo ni suuratudh dhu7aa.

    Kilichomfanya Mtume.a.w atokwe na jasho katika masiku ya baridi kali ni uzito wa Qur'an, na Allaah s.w ametangulia kusema: إنا سنلقى عليك قولا ثقيلا, kwakua ni qawli nzito ambayo lau ingeteremshwa kwa jabali lingetawanyika pamoja na ukubwa na ugumu wake..لَوْ أَنْزَلْنَا هَذَا الْقُرْآنَ عَلَى جَبَلٍ لَرَأَيْتَهُ خَاشِعاً مُتَصَدِّعاً مِنْ خَشْيَةِ اللَّهِ ... hii yatuonesha himma ya Mtume s.a.w ni ya hali ya juu kushinda hata majabali ndio akaweza kustahmili uzito huo wote.... Mungu amrahamu hassaan bin thaabit mshairi wa Mtume s.a.w aliposema: له همم لا منته لكبارها ... وهمته الصغرى أجل من الدهر , Mtume s.a.w ana himma zisokua na kiasi ukubwa wake, na himma yake ndogo kabisa ni kubwa kuliko ulimwengu.

    wallaahu a3lam

    ReplyDelete
  2. Pengine ni ulize wah'yi ninini..?naziko ayna ngapi...?na wahyi yatoka kwanani yaenda kwa nani..?

    Baada yakupata idhni kwa mashekhe zetu twa tawakkala 3ala Allah ..wahyi katika lugha wasema kuwa ni kujulisha kitu chochote kwa siri kwa ishara au kwa kuandika au kwa kuishiri kwa jicho alie kusudiwa akafahamu bila yawengine kufahamu zote hizo huitwa wahyi ki lugha .. ama istwilaahi au ki sheri3a ni Allah kumjulisha Mtume wake. japo kuna ikhtilafu katika ta3rifu yake yaani definition yake..

    Anwa3i yani sampuli za wah'yi 1 ni mtume kuota makusuio ya mtume hap ni mtume yeyote ..kama ilivo katika hadithi kuwa ndoto za mitume ni wah'yi " رؤيا الأنبياء وحي " .. hata nabi ibrahiim alayhissalaama ilipo kuja amri kumchinja mwanae aliona usingizini............ إني أرى في المنام أني أذبحك 2 nimalaika kumjiya mtume kwa sura ya mtu mwanamume kama katika hadithi ya jibriil idhtwala3a alayna rajulun shadidu bayaadhitthiyaab..mpaka mwisho wahadithi mtume.s.a.w akauliz mwamjuwa aliye kuja ninani wakasema maswahaba la mtume s.a.w alikuwa ni Jibri amewajiya awafundishe didni yenu. فإنه جبريل ، اتاكم يعلمكم دينكم "رواه مسلم . na ayna hi ndio moja katika mbili zilo tajwa hapo juu nakatika sampuli hii mtume alikifahamu kwa sahali hapati taabu kama ayna ambayo itayo fuatiya 3 njiya ya tatu ya wahyi nayo pia ime tajwa hapo ju katika hadithi na sidi mubarak ameeleza kwa uzuri hapo juu ..nikumjia wahyi kama sauti za kengele مِثْلَ صَلْصَلَةِ الْجَرَسِ na maswahaba walikijuwa wahyi huu ikiwa mtume s.a.w ameeka mkono ju ya swahaba basi mkono wa mtume s.a.w utakuwa mzito 4njiya ya nne ni Allah amlete wahyi moja kwa moja kwa Mtume s.w.a bila ya waasitwah nahapa ndipo zinapoa patikana hadithi za qudsiiyy 5njiya ya tano ni malaaika amjie kwa sura zake yani kwa sura malaika njiya ya sita ninjiya ambayo kwamba mtume yuwatukuwa kwa Allah s.w.t kama zlipo faridhishwa swala tano Allah s.w.t asema وما كان لبشر أن يكلمه الله إلا وحيا أو من وراء حجاب أو يرسل رسولا فيوحي بإذنه ما يشاء

    Je, wah'yi ni utokao kwa Allah kuenda kwa Mtume s.a.w au unaweza kuenda kwa mtu wa kawaida na je unaeza kutoka kwa asie Allah s.w.t wah'yi ukitwaliqiwa yani neno la wah'yi bila ya taqyidi yani kufungana nakitu chochote basi huo ni wah'yi unaotoka kwa Allah kuenda kwa Mtume kama katika aya hi .. انا أوحينا اليك كما أوحينا الى نوح..hakika sisi tumekuletea wahyi kama tulivo mletea Mtume Nuh a.s ama ukitoka wahyi kutoka kwa Allah kuenda kwa asiye mtume basi huitwa ilham nayo ni ilmua ambayo Allah s.w.t huiweka katika moyo wa mja wake amtakae . Allah s.w.t asema : «إذ أوحينا إلى أمك ما يوحى» Na pindi tulipo mletea wah'yi yaani ilhaam kama walivo tafseer wanazuoni ..navile vile inaezakuja wahyi katika Qur'aan kwa maana ya wasiwasi wa shaytwaani kuotoka kwa mashaytwani kwenda kwa marafiki zao وإن الشياطين ليوحون إلى أوليائهم .. nahakika masheytwani huwatiya wasiwasi marafiki zao ... kama ilivo tajwa katika tafseer jalaleyni na baydhwawi.. nayaeza ikaja kwamaana nyengine. Wallahu a3lam ikiwa nimekoseya kwa niliyo nuku basi mashekhe wataeka sawa duwa zenu kwa wingi.

    ReplyDelete