Bismillah alRahman alRahiym
Kwa mujibu wa mafunzo ya kiislamu
ni muhimu (bali ni wajibu) kuyaelewa mas-ala kabla ya kuyatolea hukumu.
Wanachuoni wa Usuul wanasema kuelewa mas-ala ni nusu ya jawabu. Nasi kabla ya
kutoa hukumu juu ya mas-ala ya maulidi ni vizuri tukawa na mtazamo sahihi juu
ya kadhia nzima kabla hatujatoa hukumu. Quran inatuonya kuwa kusema kuwa hili
ni halali na hili
ni haramu bila ya kuwa na elimu ni kumzulia Mungu, na hili litapelekea katika adhabu kali mbele ya Mungu.
ni haramu bila ya kuwa na elimu ni kumzulia Mungu, na hili litapelekea katika adhabu kali mbele ya Mungu.
Kimsingi Maulid ni
kumsherehekea Mtume swalallahu aleihi wa salaam kwa ujumla na hususan kusherehekea mazazi
yake. Hii ndiyo nadharia ambayo tunaiangalia, na kwa ujumla sherehe hizi
zinachukua sura mbalimbali, katika miji na nyakati tofauti. Hivyo swala
lililoko mbele yetu ni kuona kamajambo
hili linafaa au linakubalika kisheria au la.
Katika kulijibu swali
hili kwanza napenda nikubaliana na baadhi ya wapinga maulid kuwa baadhi ya
mambo yafanyikayo katika baadhi za sherehe za maulid, ni haram na mara nyingi
huwa yanakemewa na baadhi ya masheikh wakati wa hizo maulid. Mfano ni kuchanganyika
wanaume na wanawake, katika baadhi miji wakati wa mawlid, sidhani kama yuko
mtu atakayejuzisha hilo...
Naam, tukirudi katika
mas-ala yetu ya msingi nitatoa hoja katika makala hii, (japo kwa ufupi)
kuonyesha kuwa swala hili kama lilivyo katika mfumo wa sasa ni kweli
halikuwepo wakati wa mtume, lakini kutokuwepo kwake hakulifanyi kuwa ni baya na
haramu. Hii ni kwa sababu sio kila ambacho hakikuwepo wakati wa Mtume
kinakuwa hakifai. Sote tunajua kuwa kuna mambo mengi ya kidini ambyo hayakuwepo
wakati wa Mtume lakini kutokana na umuhimu wake na kwa vile yalivyo na mashiko
sahihi ya kidini basi yalikubaliwa na wale waliokuwepo wakati ule na yakawa ni
sehemu ya dini. Nitatoa mifano baadaye...
Lakini kwa sasa napenda
nionyeshe kuwa kuwa kuna misingi ya kidini inayofanya swala zima la maulid liwe
ni lenye kukubalika na ni sehemu ya dini. Nitatoa hoja kutoka katika Qur'an na
Sunna na hoja za kiakili na kilugha kuthibitisha usahihi wa madai yangu.
Baadaye nitaonyesha japo kwa uchache udhaifu wa hoja za wale wanaokana Maulid
kuwa ni sehemu sahihi ya dini.
Katika Surat Yunus aya
ya 58, Allah anasema: ''Sema: 'Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na kwa rehema zake
.... Basi na wafurahi kwa hayo. Haya ni bora kuliko hivyo wanvyovikusanya' ''.
Hoja hapa ni kuwa kupatikana kwa rehema na fadhila za Allah ni sababu kubwa kwa
waumini kufurahi. Pia hili la kufurahi na kufanya sikukuu kwa ajili ya
kushukiwa na aya ya MwenyeziMungu na rehema zake na fadhila zake limetajwa tena
katika Surat al Maidah aya ya 114, kwenye dua ya nabii Isa ya kuomba chakula
kutoka mbinguni '... ile kiwe sikukuu...' Kwetu sisi waislamu hakuna rehema na
fadhila kubwa kutoka kwa Mungu na aya kubwa ya Allah kwa wanadamu zaidi ya
majilio ya Mtume. Na Maulid ni moja ya namna ya kuonyesha furaha yetu kwa hilo.
Allah anasema لقد مَنّ
الله على المؤمنين إذ بعث فيهم رسولاً من أنفسهم
"Na Allah amewafanyia
fadhila waumini kwa kuwapa mtume toka miongoni mwao"
Tunaona pia katika
vitabu vya hadith Mtume swalallahu aleihi wa salaam alipofika Madinah alikuta Mayahudi wakifunga
mwezi kumi Muharram , akauliza kwa nini wao wamechagua siku hiyo kufunga? ,
wakajibu kwa kusema ni siku ambayo Allah alimwangamiza Fira’un na akamuokoa
Nabii Musa(A.S), hivyo tunafunga siku hii kumshukuru Allah Subhanahu wa Taalah
kwa neema alizotujaalia Allah ambayo
kishariah inaonyesha uhalali wa kumshukuru Allah(S.T).Hoja hii imetumiwa na
Muhadith Hafidh Ibn Hajar Al Asqalani kutetetea maulid. Sisi waisilamu
tunasheherekea kwa siku
tuichaguayo , au msimu Fulani katika kila mwaka kwa njia nyingi za ibada kama
vile kusoma Quraan na dhikr(hadhara) , kuswali , kufunga , kujitolea na kufanya
swadaqa.Kwetu sisi Mtume swalallahu aleihi wa salaam ni Rahma kubwa ambayo yatufaa kuisherehekea
siku aliyozaliwa kama alivyofanya yeye kwa kufunga sisi ambao hatukumuona Mtume
swalallahu aleihi wa salaam tufanye
nini?.
Na katika hadithi sahihi
ya Mtume swalallahu aleihi wa salaam juu
ya sababu ya kufunga Jumatatu, akasema kuwa hiyo ni siku aliyozaliwa. Hii ni
ishara ya wazi juu ya umuhimu wa siku ya kuzaliwa mtume swalallahu aleihi wa
salaam , na kwamba katika kumfuata mtume
swalallahu aleihi wa salaam juhudi za
wazi ni lazima zifanyike kumshukuru Mungu juu ya hilo. Maulid ni miongoni mwa juhudi
hizo.
Mara nyingi kuna hoja
inajengwa kuwa kama jambo halikufanyika wakati wa Mtume
basi hakuna ruhusa ya kufanya jambo hilo.
Hoja hii ni dhaifu kwa sababu sote tunajua kuna mambo' mengi ya kidini' ambayo
hayakufanyika wakati wa Mtume swalallahu aleihi wa salaam lakini masahaba au wale waliokuja baada yao waliyafanya
na yalihesabiwa kuwa ni sehemu ya dini.
Mfano mzuri ni
swala ya taraweh, ambayo ni sehemu ya dini na ambayo imekuwa ikiswaliwa miaka
yote na waislamu tokea zama za Khalifa Umar (r.a) na hakuna muislamu aliyesema
kuwa hilo halifai, bali Umar alinikuliwa akisema kuwa hii ni BIDAA NZURI. Hoja
kuwa Umar alikusudia Bidaa ya kilugha ni dhaifu kwa sababu tunajua kuwa bidaa
aloikusudia ni watu kuswali tarawehe jamaa na hili ni swala la kidini na sio
swala la kilugha.
Imesimuliwa katika Sahihi
Bukhari mujaraba wa 3, juzuu 32, hadithi namba 227: kuhusu
Bida’a;
'Abdur Rahman bin 'Abd ul-Qariy anasimulia, " Nilikuwa na Umar bin
Al-Khattab usiku mmoja katika
masiku ya Ramadhan msikitini tukakuta watu wakiswali katika makundi tofouti tofauti
wengine wakiswali kivyaovyao(pekee yao)
na wengine kwenye kigenge kidogo
cha watu chini ya Imam mmoja, Sayidna Umar akasema, "Kwa rai yangu ningependa
kuwakusanya hawa watu wote wakasali chini ya Imam mmoja na hivyo wasali
chini ya imam huyo.
Siku iliyofuata
alipowakuta wanaswali kwa pamoja akafurahi na kusema…..نِعْمَت البِدعةُ هذِه
Kwa mtazamo na mujibu
wa skuli ya Kisalafiyah nafikiri hii ni bidaa ya "kilugha’’ hata sielewi wanakusudia nini kusema hivyo. Kwa
kitendo hiki na kauli ya Sayidna
Umar (R.A) uwelewo na
mtazamo wa wa Ibn, ni hawa watu wanaosema kuwa bidaa haigawanyiki
kivyovyote leo hii wakibanwa husema bidaa ya Kilugha!!!Hebu tusome wafaswaha wa
lugha na Hadith wanasemaje kuhusu neon hili alilolitumia sayidna Umar (Radhiallahu
anhu)
Hajar Asqalani
katika sherhe yake ya swahih al Bukhari anasema ya ama maneno
haya Sayidna Umar (R.A).... (Ni’mat al bida hadhihi)……
Anasema hivi;
Asili ya neno bidaa ni
kile kilichokuja baada ya mtume swalallahu aleihi wa salaam Ni moja katika kanuni za kishariah kwa jambo
lenye kuendana kinyume na Sunnah na hivyo kuwa dhwalala. Kimsingi jambo hilo kama likiwa ni zuri kisharia basi linakuwa
bidaatul Hassana, kama jambo hilo likiwa
halikubaliani na shariah basi linakuwa mustaqbaha, vilevile kama litakuwa
linakubalika na baadhi linakuwa Mubah.
Vilevile Bidaa inaweza kugawanyika katika vipengele vitano. Hapa Ibn Hajar hajatuletea hoja za bidaa ya Kilugha bali jinsi anavyoelewa neno Bidaa.
Vilevile Bidaa inaweza kugawanyika katika vipengele vitano. Hapa Ibn Hajar hajatuletea hoja za bidaa ya Kilugha bali jinsi anavyoelewa neno Bidaa.
Kilichotokea hapa
ni kuwa Umar alianzisha mwenendo mwema na hivyo yeye na maswahaba wengine
waliohusika wataendelea kupata malipo yao mpaka siku ya kiyama, kama ilivyo
katika hadithi nyingine ya Mtume swalallahu aleihi wa salaam
من سنّ في الإسلام سنّةً حسنة فله أجرها وأجر من عمل بها بعده من غير أن ينقص من
أجورهم شىء، ومن سنّ في الإسلام سنّة سيئة كان عليه وزرها ووزر من عمل بها من
بعده من غير أن ينقص من أوزارهم شىء.
Hadithi inasema:
"Atakayeanzisha mwenendo mwema "سُنَّةً
حَسَنَةً katika Uislamu atapata ujira
wake na ujira wa atakayetenda wema huo hadi siku ya Qiyaamah bila ya
kupungua kitu katika ujira wa waliotenda, na atakayeanzisha mwenenedo
mbaya سُنَّةً
سَيِّئَةً atapata madhambi yake na madhambi ya atakayetenda
madhambi hayo mpaka siku ya Qiyaamah bila ya kupungua kitu
katika madhambi yao." (Swahih al- Muslim na At-Tirmidhy
na An-Nasaaiy na wengine)
Sasa tuawaulize wale wanaonadi kila bidaa ni upotofu
na vipi je kuna Sunnah mbovu waijuayo?hadith hii huiruka sana na kujifanya
hawaitambui au kuwa hap si mahala pake. Bidaa nyingine
tuipatayo kwenye vitabu vya Sunnah.
Mbali na Tashahud
ya kawaida tuijuayo Abdullah Ibn `Umar. Alifanya nyongeza katika mwanzo
wa Tashahud (Tahiyatu) kwa kuanza kusema (Basmallah) yaani Bismillah Rahman Rahim, na mwisho
akaongeza Talbia; "labbaika wa
sa'daika wal khayru bi yadayka wal raghba'u ilayika wal `amalu" Haya yameelezwa katika
Bukhari na Muslim.
Baadhi ya Bidaa njema za
miaka ya hivi karibuni:
- Watu kukusanyika katika misikiti miwili mitukufu ya Makkah na Madinah na misikiti mingi duniani kuswali Tahajud baada ya salat Taraweh nyuma ya Imam mmoja (wakibadilisha na wasomaji mara nyingi)
- Kusoma dua ya
kukhitimisha Quraan katika swala ya Taraweh na vilevile katikaTahajud mwezi wa
Ramadhan!
- Kufanya mwezi 27 siku ya kukhitimisha Quraan katika misikiti miwili Makkah na Madinah
- Muadhin kusema maneno Allah akulipeni malipo mema(bora), baada ya kumaliza Taraweh na Qiyam katika misikiti miwili ya Makkah na Madinah
Hatuyakatai haya kwani twajua msingi wake ni Bidaa iliyo nzuri , ila twasema kuwawale wapingao Maulid , hakika hawajioni na hujifunga wao wenyewe dhidi ya kauli zao wenyewe kwa kusema kuwa kila ambalo hakulifanya Mtume S.A.W au swahaba zake ni upotofu, kwa mantiki hii basi wao pia wako katika upotofu kwa kuanzisha haya na mengineyo...
Au Bidaa hizi ni za ‘’Kilugha(lughawiyah)?
Maana ya
كُلُّ بِدعةٍ ضَلالةٌ:
Hafidh Ibn Hajar
Al Asqalani, aliyefanyia sherhe Al Bukhari, anatuambia
kuhusu bidaa, " Chochote kile ambacho hakikuwepo wakati wa mtume S.A.W kinaitwa Bida’a
lakini kuna Bida’a njema na Bida’a mbaya. Abu Na'im, anasimulia
kutoka kwa Ibrahim Al Junaid, asema , "Nimemsikia Ash-Shafi'i
anasema, "Bida’a zipo za aina mbili , bida’a njema(hasana) na chochote kile
kitakataana na Sunnah ni dhwalalah(ni bida’a mbaya) na bida’a mbaya (dhwalala)
Suali linakuja Maulid
yapingana na na Quraan na Sunnah?
Al-Hafidh al Bayhaqi,
Manaqib As-Shafiy(1: 469)
"Al Muhadithatu min umuri
darbani alduhuma ma uhitha yukhalifu kitaban aw sunatan aw atharan aw ijma’an
fa hadhihi al bidaatul dhalala wal althaniyatu ma uhdidha min khairi la khilafa
fihi li wahidin min hadhihi wa hadhihi muhdathatun ghayru madhmuma"
Imam Albayhaqi
anasimulia katika Manaqib Ash-Shafi'i ya kwamba Ash-Shafi'i anasema
kuwa , Bidaa zipo za aina mbili , ile ikataanayo na Quraan na Sunnah(Bidaa’t
dhalala) na Bidaa nzuri ni ile ambayo haipingani na hivi(yaani Quraan na Sunnah)
Al `Izz bin Abdussalam
anasema mwisho wa kitabu chake , Al Qawa'id,
Bidaa imegawanyika
katika ulazima, ilokatazwa , inayopendekezwa, isokubalika na inayokubalika, na
ukitaka kuifahamu basi angalia ile inayopishana na shariah (Quraan na Sunnah)
Pamoja na kwamba
iliwachukua waislamu takriban karne nne kuzinduka kuhusiana na swala hili la
maulid, hiyo siyo hoja kuwa jambo hilo linakwa haram, kwani kuna rekodi
sahihi za wanachouni wengine kabla ya hapo kujihusisha kwa namna moja au
nyingine kumsifu mtume na kumshangilia, hivyo maulid yanakuwa ni maendeleo
mwafaka katika mrengo huu. Na hata wale wanachuoni waliokuja baadaye
wanaohesabiwa kuwa ni wanachuoni wa mrengo wa ki-salaf, pia walijihusisha na
maulid kwa kuandika vitabu n.k kuonyesha kuwa swala hili halipingani na mafunzo
sahihi ya Mtume.
Sheikh Ibn Taymiah
baba wa Usalafiyah anasema hivi kwenye kitabu chake Iqtidaswiratal mustaqim
chapa ya Dar Hadith ("Majma' Fatawi Ibn
Taymiyya,") Mujaraba wa. 23, uk . 163:
"fa-ta'adhwm al-Maulid wat-tikhaadhuhu mawsiman qad yaf'alahu ba'ad an-naasi wa yakunu lahu fihi ajra`adhwim lihusni qasdihi ta'adhwimihi li-Rasulillahi, swalallahu aleihi wa salaam"
"fa-ta'adhwm al-Maulid wat-tikhaadhuhu mawsiman qad yaf'alahu ba'ad an-naasi wa yakunu lahu fihi ajra`adhwim lihusni qasdihi ta'adhwimihi li-Rasulillahi, swalallahu aleihi wa salaam"
"Kusheherekea na kuitukuza siku ya mazazi ya Kipenzi Muhammad
S.A.W na watu kufanya ni msimu wa
sherehe, kama wafanyavyo baadhi ya watu ni
nzuri na wanapata ujira mkubwa
katika kutokana na nia yaonjema
kwa jambo hili la kumuenzi Rasullulah swalallahu
aleihi wa salaam"
Ibn Tay'miah anaendelea
kwa kusema katika kitabu chake hicho, ukurasa wa 266 sentensi ya 5 toka
chini Kwa jinsi watu wanavyofanya wakati wa sherehe hizi za maulid kama ni
ushindani dhidi ya wakiristo wafanyavyo wakati wa kirisimasi kusheherekea uzao wa
Nabii Issa aleihisalaam au ni hali ya kuonyesha mahabba kwa kipenzi chetu Muhammad swalallahu
aleihi wa salaam na dalili ya mapenzi
juu ya Mtume wetu kipenzi swalallahu aleihi
wa salaam, Allah atawalipa malipo mema kwa ijtihad yao hiyo mbali ya kuwa kitendo hiki ni
bida’a. Hii ni kutokana na mapenzi yao na nia yao njema
kwa suala hili. Ibn Taymiah
anaendelea kusema, "Twajua kuwa Maulid haikuwahi kufanywa na salaf,
wangeifanya kama wangetaka kwani hakuna kipingamizi chochote cha kisharia
kilichowakataza waisifanye maulid"
Kipande hiki na vingine
vingi mno katika vitabu vya Ibn Taymiah na wengineo vimeondoshwa kwa
makusudi kabisa na Masalafiyah( Mawahabi) kama wafanyavyo kwenye vitabu vingi vya
Sunnah na maandiko ya kihistoria kupotosha ummah. Kuna editor wa Kiwahabi kwa jina Muhammad Hamid
al Fiqqi , ameandika maneno yafuatayo kwenye sherhe yake chini kwa mshangao
mkubwa sana eti…"kayfa yakunu lahum thawabun ala hadhaa…?Ayu ijtahadun fi
hadhaa??"
Ibn Jawz ameandika kitabu cha
mashairi kuhusu mazazi ya Mtume (Maulid), Ibn Jawz ameandika kitabu cha maulid
kwa mashairi kwa kuanza na beti hii….Alhamdullilah
al-ladhiy abraza ghurrati aru’si al hadharat subhan Mustanira……
Na Imam Ibn Hajar
al Asqalani ameandika Katika kitabu al Durar al kamina fi ayn al mi’at al
thamina anasimulia kuwa Ibn Kathir Muhadith na
pia mfuasi wa karibu mno wa Ibn Taymia ya kuwa kabla ya umauti wake Ibn Kathir
aliandika kitabu kinaitwa Maulid Rasullullah. Kitabu kimeandika juu ya ruhusa
ya kuwepo na kufanywa maulid na kuonyesha kuwa
hakuna ubaya kusherehekea mazazi ya Mtume swalallahu aleihi wa salaam.
Kwa maelezo zaidi ya Bida’a3
fuatilizia mfululizo wa Video za Al Akh AlKarim Al-Habib Mbarak Ahmed youtube
au kwenye viunga vya blog hii (video za kiswahili)
Wa Billah Tawfiq
taja vitu ambazo haziukua wakati wa mtume na zipo sasa ambazo nikatika dini
ReplyDeleteIlm al Hadith
ReplyDelete